“SANCTIFICATION IS IN YOU – IT IS A PERSON HE LIVES IN YOU.”
Utakaso wako umeingia ndani- Yeye anaishi ndani yako !
1 Wakorintho 1:30
“Mungu ndiye chanzo cha uzima wenu katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu na haki na utakaso na ukombozi,”
Hapa tuna ona ya kwamba utakaso wetu umo ndani ya Kristo, na wakati unapo okoka basi hapa anaishi ndani yako , kwa hivyo utakaso wako upo ndani mwako .Tena ni utakaso ni mtu , yaani Kristo anaishi ndani yetu .
Je umewahi kuingia kwa nyumba ingine mara moja au zaidi maishani mwako?Je ilikupasa wewe mwenyewe kusafisha ile nyumba kuhakikisha ya ilikuwa safi kabla ya kuingia na jamii yako kukaa ndani mle ?
Hi ni picha mzuri ya yale Mungu alifanya kabla aingie ndani mwako. Kuhakikisha nyumba Yake – wewe – imekuwa safi kabisa ,Alisafisha nyumba Yeye mwenyewe. Kusafisha kwake hakungekuwa mzuri sana – ila tu ndani damu ya Yesu ingefanya hiyo kazi kikamilifu .
Hii ni habari njema ! Wewe umesafishwa na ni takatifu – u matakatifu maana Mungu Matakatifu ana ishi ndani yako. Waef 1:4 inasema tu “ Kwa maana alituchagua katika Yeye kabla ya kuumbwa ulimwengu ili tuwe watakatifu na bila lawama mbele Zake.
Je lipi tunda la jambo hili kwamba wewe tayari umefanywa safi na Yeye, na sasa Yeye anaishi ndani yako? Hii barua ya habari njema ina mafundisho kuhusu
utakaso,somo ambalo kwa wengine limekuwa mzigo na sababu ya kuhukumu. Walakini, Yesu alisema hakuja kuhukumu ila ni kuokoa, na Mzigo ni mwepesi.Jinsi tumeona katika maeneo baada ya eneo , Yesu mwenyewe jawabu lake na sululisho. Je inaweza kuwa sawa na utakaso? Na tunaweza kumwomba Mungu kwa ya kuongezeka kwa undani na ufunuo tunavyo weza kujisomea mafundisho haya yaliyopo katika barua hii .
Atakufinyanga Tena
Yeremia 18:1-4
Maombi :
Yeremia 18:1-4
Neno hili ndilo lililomjia Yeremia , kutoka kwa BWANA, kusema,
Tambua : NENO lilimjia ( Bwana , kwa udhahiri alimtembelea Yeremiah)
Tambua : Yeremia anatambuliwa na Mungu… kujulikana na Mungu
Tambua : Hi inadhirisha uhusiano kati yao.
Tambua : Ina maanisha Yeremia ni mtu wa kupokea. Ana weza sikia kutoka
kwa sauti ya Bwana
Tambua : Waebrania : 13:8 Yesu Kristo ni yeye yule, jana, leo na milele.
Malaki 3:6 Kwa kuwa mimi , BWANA, sina kigeugeu;
Tambua : Alitaka kusema na watuWake , kwa hivyo Angali ana nena leo hii
Tambua :Yesu anasema habari ya Masikio yenye kusikia.
Marko 4:23 Mwenye masikio na asikie!"
Alisikia nini ? Maagizo .
Je Mungu anaweza kuagizo wewe na mimi? Je anaweza kutuhimiza ,Je anaweza kutia nuru kwa NENO Lake ?
Ujumbe :
2.Ondoka , ukashuke mpaka nyumba ya mfinyanzi, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
Tambua: Ondoka ! amka Yeremiah! Wewe hauko mahala sawa.Unahitaji kufanya kitu.Unahitaji kuenda pale ninapo weza kukutana na wewe .Enenda mahala nitakapo kufundisha.
Tambua : MPAKA , tuondoke hatawezi kufika katika Nyumba ya Mfinyanzi.Mungu hawezi kutuleta nyumbani Mwake , Ni sharti tu ondoke na tuende! Lazima tumsikize Yeye na Tuende anapo tuongoza sisi.
Kwa nini Anatutuma mahali Anako tutuma ?
Kupokea toka kwake yale hatuwezi kupokea toka mahali pengine .
Kuona kitu anacho taka kutuonyesha ambacho hatuwezi kuona
kwengineko .
Kukutana na sisi ni mahala pa Upako wake maalum.
Kufanya kitu anacho taka kufanyia wengine .
Kushiriki ujumbe wake na wengine
Kutufanyia matendo mema .
Tambua: Ni sharti tuende MWENDO HUU WOTE MPAKA HUKO. Hatuwezi
kuenda nusu tu na tuwe Nyumbani mwa Bwana !
Tambua : Mungu alikuwa na sababu maalum kwa nini alitaka Yeremia aende
katika Nyumba ya Mfanyanzi . Alitaka ampe ujumbe wa mfano., ule
ambao ange UONA. Tuna hitaji macho ya kuona pia masikio ya
kusikia .
Kumbukumbu la Torati 29 :4 lakini BWANA hakuwapa moyo wa kujua , wala macho ya kuona, wala masikio ya kusikia , hata leo hivi.
Yohana 5:19-20 :
19.Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
20.Baba ampenda Mwana, na humwonyesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonyesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
Tambua : Yeremia ALIPOFIKA BILA SHAKA Mungu akazungumza na Mtumishi
akasikia
Tambua: Kwa Yeremia alikuwa na chaguo , la kutii na kupokea au kutotii na asijua
Mungu alikuwa na jambo lipi juu yake ..Hii ni kutosha kunifanya mimi
nitii.Ninataka kujua Mungu ana jambo lipi katika hasina yake kwa ajili
yangu!
Tambua : Kuna ahadi hapo Mungu anasema ata msababisha Yeremia kusikia !!!
Anaweza kufanya hivyo kwetu sisi tunapo weza kuchagua kumtii Yeye.
Tambua: Tuko karibu kuona Zawadi ya Yeremia aliye chagua kutii maagizo ya Mungu
Wake .
Tambua : Tuko karibu kuona hadithi ya UPENDO WA MUNGU ukifunguliwa mbele
ya macho yetu !
3. Basi ni shuka mapaka nyumbani mwa mfinyanzi na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu.
Tumbua : Mfinyanzi katika hadithi hii ni Baba Mungu . Yeye anafinyanga
chombo, Yeremia aliweza kuona hali ya upitilzo wa Mwanadamu, aliye
chombo .
Tambua : sisini kazi ya Mikono ya Mungu. Waef 2:10 Sisi ni viumbe vyake
Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya
kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
Tambua: Yeye ni Mwanzo tena mwisho . Ufunuo 21:6
Kisha akaniambia, "Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
Tumbua : Tunayo ahadi yake ya kwamba alicho anza ata kamilisha
Wafilipi 1:6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwanba yeye aliyo anza kazi moyoni mwenye ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu .
4. Na chombo kile alikuwa akifinyanga, kilipoharibika mkononi mwake yule mafinyanzi,alikifanyiza tena kuwa chombo kingine, kama alivyoona vema yule mafinyanzi kukifanya.
Tambua : Chombo alichokifanya …. Mkristo .alitengenezwa na Mungu . Sura ya
mfano wake .
Tambua:Tuliumbwa kwa udongo. Ingekuwaje kwamba hili umbo lingekuwa udongo.Udongo unafinyangwa, unayo rangi, kitu kinacho weza kufanyazwa .Udongo hauwezi kujiumba . Ila sharti upokee mshurutisho kutokana na vitu vilivyo karibu nao .Mungu alimwumba mwanadamu toka kwa mavumbi ya nchi kwa mikono Yake .Yeye ndiye aliweza kuwa bayana ya kufanya umbo la mwanzo la chombo hiki . Yeye ndiye atakaye kuwa bayana ya kufanya uamuzi wa mwisho juu ya chombo hiki .
Tambua : Mavunbi HAYAWI KITU ila mavumbi MPAKA YEYE( mfinyanzi
anapo ushika na kuufanyiza. Shukuru Mungu kwa mguso wake.
Tambua : Mungu anataka KUGUSA watu Wake
Tambua : Mungu ALITUUMBA SISI KWANZA , alafu Akapuliza UHAI ndani yetu,
na ROHO WAKE akatufanya kuwa haya hai. Huo uhai sharti ulitakikana
uwe wa milele, lakini dhambi iliweza kuharibu na kulete mauti .
Tambua : Tangu dhambi na mauti zimeingia katika dunia lazima tukabiliane na mvuto mwingine juu ya maisha yetu, mzongo kuliko Mungu . Licha ya kuwa mikononi Mwake tukiwa Wake, tungali twaishi katika mwili ,duniani hapa .Tuna kumbwa na mzongo katika pande zote .Misiba hutukia.Vipande na sehemu ya yaliyopita wakati mwingine yamesababisha sisi kuvunjika moyo na kukosa kufanya kazi vizuri na tuna patwa na dhambi .Ni wakati tunapo umika KIKAMILIFU mikononi Mwake ndipo tunakuwa salama
Tambua : Kila chombo ni cha kipekee . HUKUNA vyombo viwili wanavyo fanana . Kila chombo kina thamana yake . Kina mwenyewe , mfinyanzi . Sisi ni Vyombo vya Mungu Maalum .Anataka kutotoa kutoka utukufu hadi utukufu , Akivirembeshe vyombo vyetu hadi milele.
2 Wakorintho 3:18
Basi, sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa, twaonyesha kama katika kioo, utukufu wa Bwana; tunabadilishwa tufanane zaidi na huo mfano wake kwa utukufu mwingi zaidi. Hiyo ni kazi yake Roho wa Bwana.
Tambua : Udongo uliwaza kuharibiwa , Kuna uzito fulani ulioweza kuufinya
ULIPO KUWA MKONONI MWAKE .
Tambua : Wakati mwingine tunaumizwa licha ya kuwa mikononi Mwake .Tambua ahadi iliyopo hapa Ali UFANYA TENA UDONGO HUO. Hakuwacha udongo huo chombo kilicho vunjika au kilicho haribiwa . Hakuwacha kuwa bure . Hakuwacha kuwa sura mbaya na kuwa bure.
Kwa kila kuanguka,kwa kila masaibu katika maishani mwetu , kwa kila dhambi iliyo njiani mwetu , kwa kila wakati tunopo danganyika , Yeye anataka kutuumba tena , mara ingine . Sisi ni udongo ule ule , chombo kile , Lakini Atatufinyanga tena kuwa, chengine , chombo bila hitalafu , ule uhuribifu .Kila wakati kwa subira hutufinyanga sisi, na tuta remebeka zaidi katika Yeye , na uhakika zaidi, uaminifu zaidi , zaidi tukiwa na hasina , zaidi tunao stahili kuaminika kumfuata Yeye.
Ni jinsi gani Anatenda kazi kwa mapito ya njia ya maisha yetu .
Muhtasari :
Tuna hitaji KUONDOKA
Tuna hitaji KUENDA kwa Nyumba ya Mungu
Yeye ata Tunenea na Kusababisha Kusikia
Yeye ndiye Mwanzo wetu na Yeye ata enda nasi mpaka Mwisho .
Yeye hatatuwacha sisi wala kututupu .
Waeb 13:5-6
5.Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
6 Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
Kwa kila uharibisfu maishani mwetu , Yeye ata tufinyanga upya , IWAPO TUPO
MIKONONI MWAKE.
Tuna hitaji kuchagua KUDUMU KATIKA USALAMA WA MIKONO ZAKE.
Wakati wa maombi .
